Kamati ya maadili ya Shirikisho la soka nchini (TFF) inayoongozwa na Mwenyekiti Hamidu Mbwezeleni imemfungia Mwenyekiti wa matawi wa klabu ya Yanga Bakili Makele na katibu wa matawi wa klabu hiyo Boaz Ikupilika kutojihusisha na soka kwa kipindi cha miaka mitatu.
Viongozi hao pia wametakiwa kulipa faini ya shilingi milioni 2 kila mmoja kwa kukaidi maamuzi ya serikali na TFF yanayohusiana na maagizo ya kufanyika uchaguzi wa kujaza nafasi ambazo ziko wazi ndani ya klabu ya Yanga.
Viongozi hao walihojiwa na kamati ya maadili hivi karibuni wakituhumiwa kupinga mchakato wa uchaguzi wa klabu ya Yanga ulioandaliwa na TFF kwa maagizo ya BMT.