KESSY : Tunawaheshimu Wapinzani Na Tunatafta USHINDI

Mlinzi wa pembeni wa Taifa Stars na Nkana FC ya Zambia Hassan Kessy amesema kwenye mchezo wa leo dhidi ya Lesotho wachezaji wa Tanzania wanaingia na mambo mawili katika mchezo huo, kuwaheshimu wapinzani na kutafuta ushindi .
.
“Jambo la kwanza tutawaheshimu wapinzani kwa sababu wapo nyumbani, la pili sisi tunataka kuweka historia yetu, wenzetu waliweka yao lakini sisi tunataka kuweka ya kwetu.”
:
“Watanzania waendelee kutuombea tuweze kufanya vizuri.”
.
Mechi itakuwa LIVE @dstvtanzania #SS7 kuanzia saa 11:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki
🇹🇿🇹🇿#TwenzetuCameroon