Mlinda lango Ramadhani Kabwili, walinzi Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Godfrey Paulo ‘Boxer’ wametua mkoani Shinyanga kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Yanga kinachoshuka uwanja wa CCM Kambarage leo kuumana na Mwadui FC.
Wachezaji hao walikuwa kwenye timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 23 ambayo juzi iliondoshwa kwenye michuano ya kusaka tiketi ya kutinga fainali za AFCON 2019 kwa ngazi ya vijana licha ya kushinda kwa mabao 3-1 dhidi ya Burundi baada ya kufungwa mabao 2-0 kwenye mchezo wa kwanza.
Kuwasili kwa wachezaji hao, kumeongeza nguvu kwenye kikosi cha Yanga ambacho kitawakosa nahodha Kelvin Yondani na mlinda lango Beno Kakolanya ambao hawakusafiri kwa sababu binafsi.
Yanga imedhamiria kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa leo ili kuendeza rekodi ya kutofungwa msimu huu pia kuendeleza presha kwa wapinzani wake katika mbio za ubingwa, Azam fc na Simba