MAMBO ATAKAYOANZANAYO NINJE.
.
Mkurugenzi wa ufundi TFF Ammy Ninje amesema ataanza kufanyia kazi vitu vitatu vya msingi, falsafa ya mpira wetu, kuongeza makocha wenye sifa kufundisha ligi yetu ya juu, na kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni.
:
“Kitu cha kwanza nataka kutengeneza philosophy ya mpira wa Tanzania, sisi tunataka tucheze mpira wa aina gani kwa sababu wamepita walimu wengi tangu miaka ya 1980 lakini hadi leo hatuna philosophy . Nadhani hiyo ni sababu kubwa kwa nini watazania hatufanikiwi.”
:
“Tunaelekea vizuri ukiangalia timu zetu za U20 na U17 lakini tunakwama kwa sababu vijana hawapewi nafasi kwenye vilabu vyao, hicho kitu nitakisisitiza sana vijana wa U20 wacheze kwenye vilabu vyao.”
: “Kwenye club licence nitasisitiza kuwa na academies nimeshakuja na program, kwa sababu mimi nimekaa kwenye academies karibu miaka 12 naomba vilabu walete ushirikiano niwasaidie.”
:
“Nadhani tuna walimu 7 kati ya timu 20, kwangu mimi sio kitu kizuri na majukumu yangu mimi ni kuwasaidia walimu wazawa ili tupate walimu wazuri watakaofundisha timu zetu.”
:
“Wakati nipo South Africa 1996 tulikuwa na wachezaji watano wa kigeni, watatu wanaanza wawili wanakaa kwenye benchi kwa hiyo ongezeko la wachezaji wengi wa kigeni nitalikataa nataka watano kwa kuanza kwa hiyo watu wanaofikiria kusajili wachezaji wengi katika dirisha hili dogo walifikirie hilo”