
Klabu ya Singida United imemrejesha aliyekuwa kocha wake Fred Felix Minziro ili kusaidiana na Dragan Popadic kuhakikisha wanajiweka vizuri kunako Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
.
Awali Minziro aliachwa baada ya kuipandisha Singida United Ligi Kuu mwaka 2017.
.
Kocha huyo miezi michache iliyopita aliondolewa kunako klabu ya Arusha United inayoshiriki Ligi daraja la kwanza kwa kile kilichodaiwa kuwa hakuwa na mwenendo mzuri na kikosi hicho