Chikupe kuikosa Alliance Fc, Kamusoko arejea

Beki kisiki Andrew Vicent Chikupe ataukosa mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Alliance dhidi ya Yanga utakaopigwa keshokutwa Jumamosi March 02 katika uwanja wa CCM Kirumba

Chikupe aliumia katika mchezo wa kombe la Azam (ASFC) uliopigwa Jumapili iliyopita mkoani Lindi na Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Namungo FC. Matokeo yaliyoipeleka Yanga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo

Nae kiungo Thabani Kamusoko aliyekuwa majeruhi kwa wiki kadhaa amejumuishwa katika kikosi kilichosafiri jijini Mwanza kwa ajili ya mchezo huo

Mbali na Chikupe, mshambuliaji Matheo Anthony na kiungo Pius Buswita nao hawakusafiri na timu