Simba kuelekea Shinyanga leo, Okwi arudi Dar

Mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi alipata majeraha kwenye mchezo dhidi ya Lipuli Fc na kulazimika kurejea jijini Dar es salaam kwa ajili ya matibabu zaidi

Hata hivyo Okwi bado anaweza kuungana na kikosi cha Simba kwa ajili ya mchezo dhidi ya Stand United utakaopigwa keshokutwa katika uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga

Msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara amesema hatma yake itategemea na ripoti ya Daktari wa timu hiyo Dk Yassin Gembe

Wakati huo huo Simba inaondoka mkoani Singida leo kuelekea Shinyanga tayari kwa mchezo dhidi ya Stand United utakaopigwa Jumapili