
DR Congo mwishoni mwa mwezi huu itachuana na Liberia katika mchezo wa kusaka tiketi ya kutinga fainali za michuano ya AFCON 2019 itakayofanyika nchini Misri mwezi Juni
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera ndiye kocha msaidizi wa DR Congo akimsaidia Florente Ibenge ambaye pia anainoa Vita Club
Bila shaka, Zahera amechangia kwa kiasi kukubwa Makambo kujumuishwa katika kikosi hicho ambacho kimesheheni wachezaji wengi wanaocheza soka barani Ulaya