Zahera amjumuisha Makambo kikosi cha DR Congo

Mshambuliaji wa Yanga kinara wa mabao Heritier Makambo amejumuishwa kwenye kikosi cha awali cha timu ya Taifa ya DR Congo chenye wachezaji 40 ambao baadae watachujwa na kubaki 23

DR Congo mwishoni mwa mwezi huu itachuana na Liberia katika mchezo wa kusaka tiketi ya kutinga fainali za michuano ya AFCON 2019 itakayofanyika nchini Misri mwezi Juni

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera ndiye kocha msaidizi wa DR Congo akimsaidia Florente Ibenge ambaye pia anainoa Vita Club

Bila shaka, Zahera amechangia kwa kiasi kukubwa Makambo kujumuishwa katika kikosi hicho ambacho kimesheheni wachezaji wengi wanaocheza soka barani Ulaya