OKWI : Atoa neno kuelekea Mechi SIMBA vs AS VITA

Mshambuliaji hatari wa Simba Emmanuel Okwi amewaita mashabiki uwanja wa Taifa kuiunga mkono Simba itakapokuwa ikichuana na Vita Club katika mchezo utakaopigwa saa moja jioni baadae leo Jumamosi

“Tunawaomba mashabiki wetu mje kwa wingi uwanjani ili kutuunga mkono.

“Siku zote tumekuwa pamoja na sapoti yenu imekuwa msaada mkubwa kwetu katika michezo iliyopita,” amesema Okwi

“Tunataka tufanye hii siku pamoja. Tunaomba mje tupambane pamoja ili tukifuzu iwe tumefuzu wote pamoja”

“Njooni uwanjani tuandike historia wote. Tumejiandaa vya kutosha na tuko tayari kuipeleka Simba hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa”