Michezo ya robo fainali kombe la FA kuanza leo

Michezo ya Robo Fainali kombe la FA (ASFC) inaanza leo ambapo michezo miwili inatarajiwa kupigwa

KMC itakuwa uwanja wa Taifa kuikabili African Lyon wakati Lipuli Fc itakuwa uwanja wa Samora kuikabili Singida United

Keshokutwa Ijumaa, Kagera Sugar itaumana na Azam Fc kwenye dimba la Kaitaba wakati siku ya Jumamosi Yanga itakamilisha michezo ya robo fainali kwa kuivaa Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa CCM Kirumba