Robo fainali ya tatu kombe la FA kupigwa leo, Yanga kesho

Michuano ya kombe la FA (ASFC) hatua ya robo fainali inaendelea leo kwa mchezo kati ya Kagera Sugar dhidi ya Azam FC utakaopigwa uwanja Kaitaba

Huo utakuwa mchezo wa tatu wa robo fainali baada ya juzi kuzishuhudia Lipuli Fc na KMC kutinga nusu fainali baada ya kushinda michezo yao

Kesho Jumamosi Yanga itakamilisha hatua hiyo ya robo fainali kwa kuumana na Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa dimba la CCM Kirumba

Mshindi wa mchezo kati ya Kagera Sugar dhidi ya Azam Fc atachuana na KMC kwenye mchezo wa nusu fainali wakati mshindi wa mchezo wa kesho kati ya Alliance Fc dhidi ya Yanga, ataumana na Lipuli Fc kwenye mchezo wa nusu fainali