FT : Alliance 1-1 Yanga, mikwaju ya penati 4-3 yaipeleka Yanga nusu fainali

Mabingwa wa kihistoria Tanzania, Yanga wametinga nusu fainali ya kombe la FA (ASFC) baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penati 4-3 kufuatia matokeo ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Alliance Fc

Yanga ilitangulia kupata bao la kuongoza kwenye dakika ya 39 likiwekwa kambani na Heritier Makambo kwa kombora la nje ya 18

Alliance Fc iliyokuwa kwenye kiwango bora ilisawazisha bao hilo kwenye dakika ya 62 kupitia kwa Joseph James

Baada ya kumalizika kwa dakika 90 huku matokeo yakiwa 1-1, changamoto ya mikwaju ya penati ikatumika kuamua mshindi

Deus Kaseke, Paulo Godfrey, Thabani Kamusoko na Haruna Moshi ndio waliofunga penati za Yanga wakati Kelvin Yondani na Mrisho Ngasa walikosa

Yanga sasa itachuana na Lipuli Fc kwenye mchezo wa nusu fainali