Wadau wa Simba Morogoro wapongezwa kwa ukarabati uwanja wa Jamhuri

Simba itaweka makazi ya muda mkoani Morogoro ikitumia uwanja wa Jamhuri kwa baadhi ya michezo yake ya ligi wakati wote ambao uwanja wa Taifa utakuwa umefungwa

Katika kuhakikisha uwanja huo unakuwa na hali nzuri, wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba mkoani Morogoro walijitolea kuufanyia ukarabati

Ukarabati uliofanywa ni pamoja na kun’goa magugu, kujaza vifusi sehemu zenye mashimo na kuotesha nyasi pamoja na kumwagilia katika kipindi cha wiki tatu zilizopita

Pia ukarabati umefanywa kwenye vyoo na vyumba vya kubadilishia nguo

Meneja wa uwanja huo John Simkoko amewapongeza Wanasimba kwa jitihada zao za kuuboresha uwanja huo

Simba itaanza rasmi kuutumia uwanja wa Jamhuri kama uwanja wake wa nyumbani kesho Jumapili itakapochuana na Mbao Fc katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara