Simba vs Mbao Fc uwanja wa Jamhuri leo

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba leo Jumapili wanashuka katika uwanja wa Jamhuri kuikabili Mbao Fc katika mchezo wa ligi utakaopigwa saa kumi kamili jioni

Simba iko mkoani Morogoro tangu juzi ikiendelea na maandalizi ya mchezo huo ambao umevuta hisia za mashabiki wa soka mkoani Morogoro na maeneo ya jirani

Kikosi cha Simba kimepania kuondoka na alama zote tatu dhidi ya Mbao Fc ambayo ilifanikiwa kushinda mchezo wa duru ya kwanza uliopigwa mwaka jana jijini Mwanza

Simba inafukuzia rekodi mpya ya kushinda michezo 10 mfululizo kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wamefanya maandalizi ya kutosha kuelekea mchezo huo na ana matumaini makubwa kuwa wataibuka na ushindi

Ushindi utazidi kuisogeza Simba karibu ya timu zilizo juu yake, Azam Fc na Yanga

Simba yenye michezo 10 ya viporo, inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 54, Azam Fc ina alama 59 ikiwa nafasi ya pili na Yanga bado iko kileleni ikiwa na alama 67

Hata hivyo Simba inaweza kuzipiku timu hizo kama itashinda michezo yake yote ya viporo