Wachezaji Yanga wapewa mapumziko ya siku moja

Kikosi cha Yanga kimewasili salama jijini Dar es salaam wakitokea mkoani Mwanza ambako jana walitinga nusu fainali ya kombe la FA (ASFC) baada ya kuifunga Alliance Fc kwa mikwaju ya penati 4-3 kufuatia matokeo ya sare ya bao 1-1

Kocha Mkuu wa vinara hao wa ligi kuu Mwinyi Zahera, amewapa wachezaji mapumziko ya siku moja kabla ya kuendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ndanda Fc

Mchezo huo utapigwa Alhamisi April 04 mkoani Mtwara kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona