
Okwi na Chama hawakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichoifumua Mbao Fc mabao 3-0 baada ya wachezaji hao kuchelewa kurudi kutoka nchini kwao walikokwenda kutimiza majukumu ya timu ya Taifa
Baada ya mchezo wa kesho, Simba itaendelea kubaki mkoani Morogoro kuendelea na maandalizi ya mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, April 06 kwenye uwanja wa Taifa