Okwi, Chama waongeza nguvu Simba ikijiandaa kuikabili JKT Tanzania

Mshambuliaji Mganda Emannuel Okwi na kiungo Mzambia Clatous Chama tayari wamejiunga kwenye kambi ya Simba mkoani Morogoro kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya JKT Tanzania

Okwi na Chama hawakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichoifumua Mbao Fc mabao 3-0 baada ya wachezaji hao kuchelewa kurudi kutoka nchini kwao walikokwenda kutimiza majukumu ya timu ya Taifa

Baada ya mchezo wa kesho, Simba itaendelea kubaki mkoani Morogoro kuendelea na maandalizi ya mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe

Mchezo huo utapigwa Jumamosi, April 06 kwenye uwanja wa Taifa