
Mkataba wa Okwi unatarajiwa kumalizika ndani ya siku 60 huku mchezaji huyo raia wa Uganda akionyesha dalili zote za kutaka kuondoka Msimbazi
Okwi anahusishwa na vilabu kadhaa vinavyoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini, Orlando Pirates na Kaizer Chiefs
Kocha Patrick Aussems alimuondoa Okwi katika kikosi kilichokwenda mkoani Morogoro baada ya mchezaji huyo kuchelewa kuripoti kambini
Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema hana taarifa kuhusu mshambuliaji huyo ambaye alikuja nchini na kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda Cranes na alicheza mchezo dhidi ya Stars
“Mimi sijui chochote kuhusiana na Okwi labda waulizwe viongozi wangu wa juu, hayupo kwenye msafara wetu huu unaoelekea Morogoro, hivyo waulizwe viongozi wa juu suala lake,”Rweyemamu alinukuliwa na Championi jana
Hata hivyo Okwi amekuwa na kawaida ya kuchelewa kuripoti kambini kila anapotoka kutimiza majukumu ya timu ya Taifa
Hali ni tofauti kwa Juuko Murshid ambaye tangu aliporejeshwa kikosini, amekuwa akiwajibika ipasavyo
Juuko alikuwa miongoni mwa wachezaji waliowahi kuripoti kambini baada ya kumalizika michezo ya AFCON
Taarifa zilizopatikana mapema leo zimebainisha Okwi amerejea na ameshatua mkoani Morogoro kuungana na wenzake