Bodi ya ligi yaahirisha mchezo wa Simba vs Biashara United

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Simba dhidi ya Biashara United uliokuwa upigwe leo katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro, umeahirishwa ili kuipa nafasi Simba kujiandaa na mchezo dhidi ya TP Mazembe

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura amesema mchezo huo umeahirishwa kutokana na Simba kukabiliwa na mchezo huo muhimu wa marudiano robo fainali ya ligi ya mabingwa

Simba sasa itachuana na Biashara baada ya kumalizana na TP Mazembe April 13 2019

Wekundu wa Msimbazi wameendelea na mazoezi kwenye uwanja wa Boko Veterans kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa Lubumbashi, DR Congo