
Katika droo hiyo, timu zitapangwa kwenye makundi sita ya timu nne nne
Droo ya makundi itafanyika kwa kuchagua timu kutoka kila chungu miongoni mwa vyungu vinne vyenye timu sita sita ambazo zimewekwa kwa kufuata ubora
Tanzania imewekwa kwenye chungu cha nne sambamba na Namibia, Guinea Bissau, Angola, Burundi na Zimbabwe
Timu zinazokuwa kwenye chungu kimoja haziwezi kupangwa kundi moja hivyo Stars haiwezi kupangwa na timu zilizotajwa hapo juu