Tutatetea ubingwa wetu ili tushiriki tena mwakani – Tshabalala

Nahodha Msaidizi wa kikosi cha Simba Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ amesema hatua ya robo fainali waliyofikia kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika imewapa somo na msimu ujao wakipata nafasi anaamini watafanya vizuri zaidi

Aidha Hussein amesema hatua hiyo imewapa nguvu ya kupambana kwenye ligi ili kuhakikisha wanatetea ubingwa wapate nafasi ya kushiriki michuano hiyo mwakani

“Tulianza kwa Kuandika Kitabu cha Historia Mpya ya Soka Letu baada ya Miaka Mingi Kupita Na Tulitegemea Kuendelea Kukiandika Kitabu Hicho Pale LUBUMBASHI Kabla ya Kukifunga Lakini Haikuwa Bahati,” Tshabalala ameandika kwenye ukurasa wa mtandao wa Instagram

“Uzuri na Utamu wa Mashindano Haya ya CAF CHAMPIONS LEAGUEUnatufanya Kama TEAM Na Mimi binafsi Kupambana Kuhakikisha Mwakani Tunarudi Tena INSHAALLAH”

Simba tayari imerejea nchini kuanza ‘mchakamchaka’ wa kula viporo katika kampeni ya kubakisha ubingwa Msimbazi