Wanachama Yanga wakumbushwa kuhakiki majina yao

Yanga iko ndani ya mchakato wa uchaguzi ambao utahitimishwa May 05 mwaka huu kwa Wanachama wa klabu hiyo kuchagua viongozi wapya

Uongozi wa Yanga umewataka viongozi wa Matawi kuwakumbusha wanachama wahakiki majina yao kwenye ‘ledger’ zilizo kwenye matawi yao

Wanachama wa Yanga pia wamekumbushwa kulipia ada za uanachama ili kuwa na sifa ya kuchagua viongozi katika uchaguzi utakaofanyika May 05

Uchaguzi utahusisha wanachama wote wenye kadi za kitabu na wale wenye kadi za posta.