Mwinyi Zahera ameanza mchakato wa kumsajili mshambuliaji hatari Roderick Mutuma (31)

Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Sc Mwinyi Zahera ameanza mchakato wa kumsajili mshambuliaji hatari Roderick Mutuma (31) raia wa Zimbabwe ambaye kwasasa anakipiga kunako klabu ya Fc Lupopo ya Congo.
.
.
Hata hivyo huenda dili hilo likaota mbawa kutokana na nyota huyo kuwa na mkataba na klabu yake mpaka Disemba 2020 huku thamani yake ikikadiliwa kuwa ni zaidi ya milioni 200.
.
.
Mutuma alijiunga na Fc Lopopo mwishoni mwa mwezi Disemba 2018 kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Nichrut ya kwao Zimbabwe.