
Zahera ambaye aliasisi zoezi la uchangiaji linaloendelea sasa, ametaka kukamilisha michakato ya usajili kabla hajatimkia kwao DR Congo anakokabiliwa na majukumu ya timu ya Taifa kuelekea fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika mwezi Juni nchini Misri
Zahera ataondoka mwanzoni mwa mwezi wa sita hivyo ametaka masuala yote ya usajili yakamilishwe mapema
Yanga inaendelea na mchakato wa kukusanya michango ya wadau wake kupitia Kamati Maalum ya uhamasishaji ambayo imemuhakikishia kocha huyo kuwa atapatiwa kiasi cha fedha alichohitaji ili kukamilisha michakato yote ya usajili
Wakati wa uzinduzi wa zoezi la kuichangia Yanga mkoani Dodoma mwanzoni mwa mwezi huu, Zahera alibainisha kuwa ana orodha ya wachezaji nane ambao wako tayari kutua Yanga
Mwenyekiti wa Kamati ya Uhamasishaji Mh Athony Mavunde amewataka, Wapenzi, mashabiki na wanachama wa Yanga waendelee kuwasilisha michango yao ili kukamilisha michakato yote kwa wakati
Kadi maalum za kuichangia Yanga ambazo zina thamani ya Tsh Milioni moja kwa kila kadi zinaendelea kutolewa, ambapo michango yote imetakiwa kuwasilishwa kabla ya April 25 2019