
Aidha matokeo hayo yametoa taswira kuwa haitakuwa kazi rahisi kwa Simba kushinda michezo yote iliyobaki
Kama Yanga itashinda michezo yote sita iliyobaki itafikisha alama 92 huku wapinzani wao wakiwa na mzigo wa kupata matokeo kwenye michezo 14 ndani ya mwezi mmoja
Yanga imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imejikusanyia alama 74 ikifuatiwa na Azam Fc yenye alama 66
Simba ni ya tatu ikiwa na alama 60
Azam na Yanga zimeshuka dimbani mara 32 wakati Simba imeshuka dimbani mara 24
Simba inakabiliwa na ratiba ngumu ya michezo ya viporo ambapo katika kipindi cha siku 15 itashuka dimbani mara sita