Kipigo cha Simba chafufua matumaini ya ubingwa Yanga

Baada ya Simba kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar kwa kuchapwa mabao 2-1, matokeo hayo yamefufua matumaini ya ubingwa kwa Yanga ambayo inaomba wapinzani wao hao wapoteze michezo zaidi

Aidha matokeo hayo yametoa taswira kuwa haitakuwa kazi rahisi kwa Simba kushinda michezo yote iliyobaki

Kama Yanga itashinda michezo yote sita iliyobaki itafikisha alama 92 huku wapinzani wao wakiwa na mzigo wa kupata matokeo kwenye michezo 14 ndani ya mwezi mmoja

Yanga imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imejikusanyia alama 74 ikifuatiwa na Azam Fc yenye alama 66

Simba ni ya tatu ikiwa na alama 60

Azam na Yanga zimeshuka dimbani mara 32 wakati Simba imeshuka dimbani mara 24

Simba inakabiliwa na ratiba ngumu ya michezo ya viporo ambapo katika kipindi cha siku 15 itashuka dimbani mara sita