Yanga yasaka alama tatu dhidi ya Azam Fc leo

Vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga leo wanashuka kwenye uwanja wa Uhuru kuikabili Azam Fc katika mchezo wa ligi hiyo

Mchezo unatarajiwa kuanza saa kumi kamili jioni

Yanga iliyojikusanyia alama 74, iko mbele ya Azam Fc kwa tofauti ya alama nane, inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kuendelea kuweka hai mbio za kuwania ubingwa msimu huu

Hata hivyo, mchezo hautakuwa mwepesi kutokana na uimara wa kikosi cha Azam ambacho tangu kimtimue kocha Hans van Pluijm kimepoteza mchezo mmoja tu

Kocha Mwinyi Zahera amesema amewaandaa wachezaji wake kikamilifu lengo lao likiwa kushinda

Amesema ni mchezo ambao wanahitaji kupambana na kuwa makini zaidi, hawapaswi kufanya makosa mengi na lazima watumie nafasi

Timu zote zitawakosa wachezaji wake waandamizi Kelvin Yondani na Aggrey Morris wanaotumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu