Azam Fc yaichapa KMC 1-0, yatangulia fainali kombe la FA

Azam Fc imefanikiwa kutinga fainali ya michuano ya kombe la FA (ASFC) baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ambao umechezwa uwanja wa Azam Complex

Bao pekee la Azam lilifungwa na Donald Ngoma katika dakika ya 75

Mchezo wa pili wa nusu fainali kati ya Lipuli Fc dhidi ya Yanga utachezwa Jumatatu, May 06 uwanja wa Samora mkoani Iringa

Mshindi wa mchezo huo atachuana na Azam Fc katika mchezo wa fainali utakaopigwa Juni 02 2019 uwanja wa Ilulu mkoani Lindi