
Simba inayoelekea kutetea taji lake la ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo, inatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam leo wakitokea mkoani Mbeya ambako wameshinda michezo yote miwili dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons
Akizungumza baada ya mchezo jana, Aussems amesema ushindi wa bao 1-0 waliopata dhidi ya Tanzania Prisons umewaweka katika nafasi nzuri zaidi ya kutetea ubingwa na kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao
Amesema atakiboresha kikosi chake ili wafike mbali zaidi ya mafanikio waliyopata kwenye michuano hiyo msimu huu
Aussems ametaja maeneo ambayo atayaboresha kwa kusajili wachezaji wapya ni eneo la ulinzi (mabeki wawili), kiungo mmoja na mshambuliaji mmoja
Aidha, Aussems amesema timu yake inakabiliwa na changamoto ya kufanya vizuri Kimataifa kutokana na ukweli kuwa haipati ushindani mkubwa kutoka timu za ndani