Aussems afichua usajili atakaofanya

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema atakiongezea nguvu kikosi chake mwishoni mwa msimu kwa kusajili wachezaji wanne

Simba inayoelekea kutetea taji lake la ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo, inatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam leo wakitokea mkoani Mbeya ambako wameshinda michezo yote miwili dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Akizungumza baada ya mchezo jana, Aussems amesema ushindi wa bao 1-0 waliopata dhidi ya Tanzania Prisons umewaweka katika nafasi nzuri zaidi ya kutetea ubingwa na kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao

Amesema atakiboresha kikosi chake ili wafike mbali zaidi ya mafanikio waliyopata kwenye michuano hiyo msimu huu

Aussems ametaja maeneo ambayo atayaboresha kwa kusajili wachezaji wapya ni eneo la ulinzi (mabeki wawili), kiungo mmoja na mshambuliaji mmoja

Aidha, Aussems amesema timu yake inakabiliwa na changamoto ya kufanya vizuri Kimataifa kutokana na ukweli kuwa haipati ushindani mkubwa kutoka timu za ndani