Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Simba dhidi ya Azam Fc umemalizika kwa timu hizo kugawana pointi baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana
Simba ilitawala mchezo huo hata hivyo Azam Fc waliotumia mbinu ya kujihami zaidi, walikuwa imara katika kujilinda
Ni matokeo ambayo bado yanaiweka Simba kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama mbili dhidi ya Yanga
Simba imefikisha alama 82 wakati Yanga ina alama 80 na Azam Fc ikifikisha alama 69
Simba inahitaji alama nane katika michezo mitano iliyobaki ili kuweza kutetea ubingwa