Simba kurejea dimba la Uhuru Alhamisi, kuikabili Mtibwa Sugar

Baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Azam Fc jana, Simba itarejea tena uwanja wa Uhuru keshokutwa Alhamisi, May 16 kuikabili Mtibwa Sugar

Katika michezo miwili iliyopita Simba imepoteza alama tano, mabingwa hao watetezi wanahitaji kushinda mchezo huo

Simba haikuwa imecheza na Mtibwa Sugar msimu huu, huo utakuwa mchezo wa duru ya kwanza na timu hizo zitarudiana May 28 siku ya kuhitimisha ligi kuu msimu huu

Katika michezo mitano iliyobaki, miwili ni dhidi ya Mtibwa na mingine mitatu ni dhidi ya Biashara United (nyumbani), Ndanda Fc (nyumbani) na Singida United (ugenini)

Simba inahitaji kukusanya angalau alama nane kuweza kutetea ubingwa wake