
Katika michezo miwili iliyopita Simba imepoteza alama tano, mabingwa hao watetezi wanahitaji kushinda mchezo huo
Simba haikuwa imecheza na Mtibwa Sugar msimu huu, huo utakuwa mchezo wa duru ya kwanza na timu hizo zitarudiana May 28 siku ya kuhitimisha ligi kuu msimu huu
Katika michezo mitano iliyobaki, miwili ni dhidi ya Mtibwa na mingine mitatu ni dhidi ya Biashara United (nyumbani), Ndanda Fc (nyumbani) na Singida United (ugenini)
Simba inahitaji kukusanya angalau alama nane kuweza kutetea ubingwa wake