Mshambuliaji wa Yanga Heritier Makambo jana aliwashukuru mashabiki wa timu hiyo kwa kumuunga mkono katika kipindi chote alichokuwa hapa nchini
Makambo aliyefunga bao pekee la Yanga katika mchezo dhidi ya Mbeya City, anatarajiwa kuondoka mwishoni mwa msimu kujiunga na Horoya AC
“Nawashukuru mashabiki kwa kuniunga mkono. Ligi haikuwa rahisi kwetu lakini mashabiki walikuwa nasi kwa kipindi chote,” amesema Makambo
“Tayari nimeshakamilisha kila kitu na Horoya hivyo nasubiri ligi imalizike nielekee Guinea nikaanze changamoto mpya”
“Ssitaacha kuwakumbuka mashabiki, wachezaji wenzangu kocha na viongozi wa Yanga kwani tumeshirikiana vizuri”
Makambo tayari amesaini mkataba wa awali klabu ya Horoya AC kinachosubiriwa ni viongozi wa timu hiyo kuja nchini kumalizana na Yanga kabla ya ITC yake kuachiwa