
Simba ilizawadiwa penati hiyo baada ya Shiza Kichuya kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari.
Simba iliendelea kutawala mchezo huo na ilifanikiwa kuandika bao la pili dakika chache kabla ya filimbi ya mapumziko mfungaji akiwa Bocco tena.
Bocco alimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Meddie Kagere aliyewatoka walinzi wa Mwadui Fc kisha kujaza majaro ya chinichini iliyomkuta Bocco akiwa uso kwa uso na nyavu.
Simba iliyonoga kwelikweli leo iliandika bao la tatu kwenye dakika ya 50 mfungaji akiwa Meddie Kagere aliyepiga shuti kali baada ya kumhadaa mlinzi wa Mwadui FC.
Bao pekee la kufutia machozi kwa upande wa Mwadui FC lilifungwa na Charles Ilafya kwenye dakika ya 81.
Bocco alitolewa nje kwa kadi nyekundu kwenye dakika ya 77 baada ya kumpiga ngumi Revocatus Mgunga.
Bocco ataukosa mchezo dhidi ya Yanga utakaopigwa Septemba 30.
Bocco aandika Historia
Mabao mawili aliyofunga kwenye mchezo wa leo yamemfanya John Bocco afikishe jumla ya mabao 100 tangu alipoanza kucheza ligi kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2008/09.
Septemba 24, 2008, Bocco alifunga goli lake la kwanza Ligi Kuu Tanzania wakati Azam FC iliposhinda 2-0 dhidi ya Toto Africa ya Mwanza.
Msimu uliopita 2017/18 ulikuwa wa 10 kwa Bocco akicheza ligi kuu Tanzania bara, katika msimu huo alifunga magoli 14 na kumfanya afikishe jumla ya magoli 98
