Aishi manula aondolewa kwenye timu ya taifa baada ya majereha kuemdelea kumsumbua

credit: @90sportsplus…

Rasmi Golkipa wa Simba Sc Aishi Manula @28_manula ameondoshwa rasmi katika kikosi cha Timu ya Taifa kitakacho cheza na Kenya katika raundi ya Pili kufuzi CHAN baada ya majeraha kuendelea kumsumbua.

Mbadala wake ameitwa aliyekuwa golkipa wa Lipuli Fc Mohammed Yusuph ambae amesajiliwa na Polisi Tanzania.

Golkeepers @taifastars_ | Juma Kaseja🇹🇿

Simba yapambanana kuinasa saini ya Justin shonga toka South Africa

credit: @sokaonline_…

HII NI FUJO ISIYOUMIZA: Chukua hii. .

.

Justine Shonga ni jina linalozungumzwa sana katika soko la usajili wa vilabu barani Afrika kwasasa. .

.

Huyu ni mzambia anayekipiga katika klabu ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini. .

.

Ubora wake umefanya aingie kwenye kinyang’anyiro cha baadhi ya vilabu barani Afrika pamoja na baadhi ya vilabu vya ulaya. .

.

Taarifa kutoka Afrika Kusini zinadai Orlando Pirates wapo tayari kumuuza nyota huyo, wababe wa Misri Al Ahly wameonyesha nia ya kumhitaji fundi huyo mwenye udambwi udambwi katika eneo lake la kushambulia. .

.

Lakini zipo taarifa ambazo inasemekana klabu ya Simba nayo imeingia kwenye shindano la kuwania saini yake. Ikumbukwe Mo Dewji ambaye ndiye mwekezaji mkuu wa klabu ya Simba aliwahi kutamka kuwa klabu hiyo ina uwezo wa kushindana na klabu yoyote Afrika kwenye saini za wachezaji. .

.

Simba Sc katika orodha yake ya usajili wa wachezaji wa kigeni imebaki nafasi moja, Unafikiri wataweza kuipata saini yake mbele ya Al Ahly ? Tusubiri tuone. .

.

Takwimu za nyota huyo katika msimu uliopita ni kama zinavyosomeka hapo juu. .

.

Gadiel Michael asajiliwa simba sc

credit: @dimbani_leo…

EXCLUSIVE: SIMBA YAMALIZANA NA NYOTA WATATU WA YANi

GADIEL Michael sasa rasmi ni mchezaji wa Simba akitokea Yanga ambapo amesaini kandarasi ya miaka miwili.

Gadiel anaungana na wachezaji wenzake wawili na kufikisha jumla ya wachezaji watatu ambao wametoka Yanga.

Wengine ni Ibrahim Ajib ambaye alikuwa nahodha wa kikosi cha Yanga pamoja na Beno Kakolanya ambaye alikuwa ni mlinda mlango wote wamesaini kandarasi ya miaka miwili.

Francis Kahata atua simba sports club

credit: @sokawaytz_…

OFFICIAL | Haijalala!! Mara Moja Baada ya kuwasili Nchini jioni hii, Kiungo wa Kimataifa wa Kenya Francis Kahata Amesaini Mkataba wa Miaka Miwili kuitumikia Klabu ya Simba SC.

.

– Kahata mwenye umri wa Miaka 27; Ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kucheza eneo la kiungo, kwasasa akiwa sehemu ya wachezaji wanaounda kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya, msimu ujao atavaa jezi ya Mabingwa hao Tanzania Bara.

.

– Amejiunga Msimbazi akitokea Gor Mahia ya Kenya ambapo akiwa kwenye klabu hiyo alishinda Kombe la Ligi Kuu mara tatu, kiungo bora wa mwaka wa Ligi Kuu ya Kenya mara mbili na mchezaji bora wa msimu 2018/2019 wa Gor Mahia.

#TPLTransferUpdates

Simba yapata chombo kingine toka Tp Mapembe

credit: @dimbani_leo…

Uongozi wa klabu ya Simba umemtambulisha mshambuliaji Deo Kanda aliyejiunga na timu hiyo kwa mkataba wa mwaka mmoja

Kanda anatua Simba kwa mkopo akitokea klabu ya TP Mazembe

Simba imethibitisha usajili wa nyota huyo aliyewahi kuitumikia timu ya Taifa ya DR Congo “Kazi ya kusajili wakali watakaohakikisha kikosi cha Mabingwa kinazidi kuwa tishio kwa wapinzani inaendelea” “Mshambuliaji raia wa Congo DR, Deo Kanda (29) amejiunga na Mabingwa wa nchi. “Kanda amesaini mkataba wa mwaka mmoja kukipiga Msimbazi akitokea TP Mazembe ambapo alikuwa mmoja wa wachezaji ambao waliiwezesha kushinda Ubingwa wa Afrika mwaka 2009, 2010 (aliifungia goli kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Esperance) na 2013 lakini pia akiwa ameshiriki Kombe la Dunia la Vilabu mwaka 2009, 2010, 2013”