Bodi ya Ligi imesogeza mbele mchezo wetu na KMC ambao ulikuwa umepangwa kuchezwa tarehe 8/11/2018 ili kupisha maandalizi ya timu ya Taifa (Taifa Stars). Pia bodi imetangaza kwamba mchezo wetu na Lipuli FC ambao ulisogezwa mbele sasa utachezwa tarehe 21/11/2018 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.