Beki wa Simba Yusufu Mlipili amesema hakuna ukweli wowote juu ya taarifa kwamba alikuwa ameikacha timu na kuelekea ‘kusikojulikana’.
Mlipili aliyesajiliwa na Simba kutoka Toto Africans misimu miwili iliyopita, hakuonekana kwenye kikosi cha Simba kwa siku kadhaa huku viongozi wa timu hiyo wakisema hawajui alipo.
“Nipo na nitaendelea kuwepo ondoeni hofu watu wangu ni uzushi tu mimi kutokuwepo mazoezini. Simba Nguvu moja kila hatua duaaa,” amesema
Hivi karibuni Mlipili alikiri kuwa na wakati mgumu kumshawishi kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems ameweze kumjumuisha kwenye kikosi cha kwanza.
Juuko Murshidi, Erasto Nyoni, Paul Bukaba na Paschal Wawa ndio waliocheza mechi nyingi za Simba msimu huu