Yanga 1-1 Reha FC : Full Time

Yanga leo imelazimishwa sare ya bao 1-1 na Reha Fc katika mchezo wa kirafiki uliopigwa dimba la Uhuru jijini Dar es salaam.

Bao la Yanga lilipatikana kwenye kipindi cha kwanza mfungaji akiwa kiungo Maka Edward.

Baada ya mchezo huo Yanga inatarajiwa kusafiri kwenda mkoani Lindi ambapo Jumapili Novemba 18 2018 itacheza mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc dimba la Majaliwa Wilayani Ruangwa

Michezo hiyo ni sehemu ya maandalizi ya kikosi cha Yanga kabla ya kusafiri mkoani Shinyanga kuikabili Mwadui Fc katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara