Full Time : Tanzania (U23) 0-2 Burundi (U23)

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania U23 kimeanza vibaya michuano ya kusaka tiketi ya kutinga fainali za AFCON 2019 U23 baada ya kulazwa mabao 2-0 ugenini Burundi.

Mabao yaliyoihakikishia Burundi ushindi muhimu yalifungwa na Shaban Mabano kwa mkwaju wa penati kwenye dakika ya 59 huku bao la pili likifungwa na Cedric Mavugo‬ ‪kwenye dakika ya 79.

Vijana hao wa Tanzania sasa wanahitaji kushinda kwa zaidi ya mabao mawili kwenye mchezo wa marudiano utakaopigwa nchini Novemba 20 2018 ili waweze kufuzu raundi ya pili.

Mshindi wa jumla wa raundi ya kwanza kati ya Tanzania na Burundi atachuana na Congo kwenye raundi ya pili