TANZANI 0-1 LESOTHO FULL TIME

Stars imeshindwa kutamba huko Lesotho baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa wenyeji, Lesotho.

Ulikuwa ni mchezo ambao Stars ilihitaji kushinda ili kujihakikishia nafasi ya kutinga fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika nchini Cameroon.

Matokeo hayo sasa yanaifanya Stars kulazimika kushinda mchezo wa mwisho dhidi ya Uganda utakaopigwa March 2019 huku ikiomba Lesotho isipate ushindi kwenye mchezo wao wa mwisho dhidi ya Cape Verde ambao watakuwa ugenini.

Lesotho ilitawala mchezo huo kwa muda mwingi huku ikikosa nafasi nyingi kabla ya kufunga kupitia mpira wa kona.

Tanzania iliyocheza kwa kujihami zaidi, ilikosa nafasi kadhaa kupitia mipira miwili ya adhabu iliyopigwa na Aggrey Morris na nafasi nyingine mbili zikikoswa na Shabani Iddi Chilunda.

Lesotho imepanda hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi L baada ya kufikisha alama tano sawa na Tanzania.

Licha ya Tanzania kuwa na uwiano mzuri wa mabao, Lesotho imenufaika na sheria ya matokeo ya jumla baina ya timu hizo mbili.

Lesotho imevuna alama nne dhidi ya Tanzania iliyopata alama moja kutoka kwao.

Michezo ya raundi ya sita ndio itaamua ni timu ipi inaungana na Uganda kwenda Cameroon huku Lesotho ikiwa mbele ya Tanzania na Cape Verde yenye alama nne