Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania umri chini ya miaka 23, leo saa moja jioni kinashuka uwanja wa Taifa kuikabili Burundi kwenye mchezo wa marudiano kusakata tiketi ya kutinga AFCON 2019 ngazi ya vijana.
Vijana hao wa Tanzania tayari wako nyuma kwa mabao 2-0 kufuatia kuchapwa idadi hiyo ya mabao kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa Burundi waiki iliyopita.
Stars U23 inahitaji ushindi wa zaidi ya mabao mawili ili kuweza kutinga raundi ya kwanza.
Kila la kheri vijana wa Stars U23.