Simba Sc yaiwinda Lipuli Fc

Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba wameendelea kujifua kwenye uwanja wa Boko Veterans kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Lipuli Fc.

Mchezo huo ambao awali ulipangwa kufanyika kesho, umesogezwa mbele na sasa utapigwa Ijumaa Novemba 23 kwenye uwanja wa Taifa.

Baada ya mchezo huo Simba itaendelea na maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa hatua ya awali dhidi ya Mbabane Swallows unaotarajiwa kupigwa Jumatano ya Novemba 28.

Wachezaji waliokuwa kwenye timu za Taifa wanatarajiwa kuanza kuwasili kikosini leo kuungana na wenzao ambao wamekuwa wakiendelea na mazoezi chini ya kocha Patrick Aussems