Kocha mkuu wa klabu ya @yangasc Mwinyi Zahera amefunguka kuhusiana na kutomtumia mshambuliaji wake Ibrahim Ajibu katika mchezo wa leo dhidi ya Mwadui Fc.
.
.
Kocha huyo amesema hakuridhishwa na mahudhurio ya nyota huyo wakati yeye akiwa kwenye majukumu ya kukinoa kikosi cha timu ya Taifa ya Congo akiwa kama kocha msaidizi.
.
.
Aliongeza kuwa kila siku kocha msaidizi wa Yanga alikuwa akimtumia majina ya wachezaji wote ambao walikuwa hawafiki mazoezini na Ajibu hakuhudhuria siku 4 hivyo ni bora afungwe akiwa ametumia wachezaji wanaofuata kile anachoagiza kuliko kucheza ambao hawana nidhamu. .
.
Mchezo huo umemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 huku nyota wake muhimu Ibrahim Ajibu na Deus Kaseke wakishuhudia mechi hiyo Jukwaani
.
#sokaonlineUpdates