Yanga yajitapa kufanya maajabu msimu ujao

credit: @simbamakini…

YANGA YAAHIDI KUFANYA MAAJABU AFRIKA

Uongozi wa klabu ya Yanga umejinasibu kufanya vizuri katika michuano ya klabu bingwa Afrika (CAF) msimu ujao kuliko ilivyowahi kufanya misimu iliyopita.

Yanga tayari imetuma CAF majina 26 ya wachezaji jana ambayo imewasajili kwa ajili ya michuano hiyo.

Kaimu Katibu mkuu wa klabu hiyo, Dismas Ten amesema kwa wachezaji waliowasajili msimu huu wana matumaini ya kufanya makubwa katika michuano hiyo ya CAF pamoja na ligi ya nyumbani. “Jana tumetuma majina 26, CAF ya wachezaji ambao tumewasajili msimu huu, matumaini yetu ya kufanya vizuri ni makubwa sana,” alisema Ten.

Marcelo asaini yanga

credit: @sokawaytz_…

OFFICIAL | Klabu ya Yanga SC Imethibitisha kukamilisha uhamisho wa Beki wa kushoto kutoka Zanzibar katika klabu ya Malindi FC, Muharami Issa “Marcelo” kwa Mkataba wa Miaka Mitatu..

.

– Kama kumbukumbu unazo mdau, Beki huyo Alitambulishwa na Klabu ya Singida United siku Sita zilizopita kwa Mkataba wa Miaka Mitatu Pia… lakini hii leo kafanyiwa vipimo vya afya na Kusaini Mkataba Mitaa ya Jangwani na kupewa Jezi Namba Mbili kabla yake ilikuwa ikivaliwa na Gadiel Michael Mbaga aliyemaliza Mkataba na Mabingwa hao wa Kihistoria..

#TPLTransferUpdates #TPLUpdates

Ajibu atoa mazito kwa mashabiki wa yanga

credit: @sokawaytz_…

– Aliyekuwa Kiungo Mshambuliaji wa Klabu ya Yanga SC, Ibrahim Ajibu amewashukuru Mashabiki na Viongozi na Benchi la Ufundi la Klabu hiyo Baada ya kukamilisha usajili wake wa kujiunga na Watani zao, @simbasctanzania, Ajibu ameandika katika Mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

:

##Repost

Hakika Ilikua miaka miwili bora sana kwangu, ndani na nje ya uwanja, Yanga ilikua sehemu ya familia yangu.

Nitoe shukrani zangu za dhati kwa viongozi, benchi la ufundi, wachezaji na mashabiki wote, kwa kuniamini na kuniunga mkono katika kila jambo.

Ni mengi nimejifunza na nina amini yatanisaidia kunijenga zaidi kama mchezaji. Asanteni sana.

Hadi wakati mwingine tena, WananchiπŸ™πŸ»

#tetesizausajili Klabu ya Yanga Sc imerejesha nguvu zake kuwania beki wa kushoto wa klabu ya Rayon Sports Eric Rutanga endapo watashindwana na beki wake Gadiel Michael. .

.

Imeelezwa mpaka sasa Yanga Sc bado hawajamuongezea mkataba mpya beki wake ambaye anatajwa kujiunga na Simba Sc.

Simba na yanga zajitoa mashindano ya cecafa ,yatakayofanyika Rwanda mwaka huu

credit: @sokawaytz…

✍🏻 Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesisitiza kuwa mashindano ya Kombe la Kagame yatafanyika kama ilivyopangwa licha ya vilabu kujitoa kwa Sababu Mbalimbali; Mabingwa wa Tanzania, Simba SC, walikuwa wa kwanza kutangaza kujitoa katika Mashindano hayo wiki iliyopita, na leo Jumapili wapinzani wao, Yanga SC pia wamethibitisha kuwa hawatoshiriki katika mashindano hayo ya kikanda.. Jana Mabingwa wa Burundi, Agle Noir FC waliandika barua ya kujitoa.

.

– Mechi za Mashindano haya zinatarajiwa kufanyika jijini Kigali, Rwanda kuanzia Julai 7 mpaka Julai 21..

πŸ—£ (Simba na Yanga) “Haishangazi hata wanapopigwa katika mashindano ya CAF, mara zote hupoteza kwa 5-0 au hata 6-0, hatufadhaiki wala haitukwamishi kwa kujitoa kwao”… Alisema Musonye ambapo Pia amesisitiza kuwa tayari wana timu kadhaa kutoka Kenya, Uganda, Rwanda na DR Congo ambazo zitakuja na kujaza nafasi hizo timu mbili za Tanzania.

πŸ—£ “Mashindano hayawezi kushindwa kufanyika kwa sababu ya Yanga na Simba hawapo, na tayari tumezungumza na timu Mbalimbali kuja kushiriki badala yao, Lengo letu ni kuwa na mashindano ya timu 16 na tutasimamia yawe hivyo” Musonye amesema.

.

✍🏻 Zesco United ya Zambia, AS Vita Club na DC Motema Pembe za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wao tayari wamethibitisha ushiriki wao pamoja na Azam FC ya Tanzania… Mashindano huleta timu kutoka Kenya, Rwanda, Burundi, Djibouti, Eritrea, Sudan, Somalia, Sudan Kusini, Ethiopia, Uganda, Tanzania na Zanzibar… Mshindi wa mashindano haya atarejea nyumbani kwake na kitita cha pesa ya thamani ya US$30,000..

#Updates #kagameCup

@Sokawaytz

Kamusoko aitwa Kikosi cha Zimbabwe Afcon

credit: @sokawaytz…

– Hongera kwao Viungo mahiri, @kamusoko_13 na @tafadzwakutinyu kwa kuwepo katika Kikosi cha mwisho cha Wachezaji 23 ambao watapeperusha Bendera Zimbabwe katika fainali za Mataifa ya Afrika AFCON mwezi huu nchini Misri.. Vijana hao wa kocha Sunday wapo kundi La A pamoja na mataifa ya Uganda, DR Congo na wenyeji Misri.

#TotalAFCON2019 #AFCON2019