Mabingwa watetezi, ligi kuu ya Tanzania Bara, Simba wamelazimishwa suluhu ya bila ya kufungana na timu ya Lipuli FC kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Kocha wa Lipuli Fc Selemani Matola ameendeleza ubabe dhidi ya timun yake ya zamani Simba huo ukiwa mchezo wa tatu timu hizo zinatoka sare
Timu zote zilishambuliana kwa zamu lakini washambuliaji walikosa nafasi kadhaa za wazi kutokana na kukosa umakini langoni
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha alama 27 ikisalia nafasi ya tatu alama mbili nyuma ya Yanga inayoshika nafasi ya pili