FT : SIMBA 4-0 MBABANE SWALLOWS

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba wametinga raundi ya kwanza ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kibabe baada ya kuifumua Mbabane Swallows mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa leo huko Eswatini.

Simba imewaondosha mabingwa hao wa Eswatini kwa ushindi wa jumla wa mabao 8-1 kufuatia ushindi wa mabao 4-1 katika mchezo wa kwanza uliopigwa wiki iliyopita jijini Dar es salaam

Mabao mawili ya haraka haraka yaliyofungwa na Clatos Chama ‘CCC’ kwenye kipindi cha kwanza yalitosha kuwaondoa Mbabane mchezoni na kuiwezesha Simba kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0

Licha ya kuwa ugenini, Simba ilitawala mchezo huo na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga mabao.

Okwi na Kagere waliongeza mabao mengine mawili kwenye kipindi cha pili kuihakikishia Simba ushindi muhimu ulioivusha raundi ya kwanza.

Simba sasa inasubiri mpinzani wake wa mchezo wa raundi ya kwanza ambapo mchezo kati ya Nkana FC ya Zambia dhidi ya UD Songo ya Msumbiji utaamua timu itakayochuana na mabingwa hao wa Tanzania katika raundi ya kwanza.

Nkana Fc iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 kwenye mchezo wa kwanza baina ya timu hizo uliopigwa nchini Msumbiji.

Nayo Mtibwa Sugar imetinga raundi ya kwanza ya michuano ya kombe la Shirikisho baada ya kuilaza Northen Dynamos kwa bao 1-0

Mtibwa imefuzu kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-1