SIMBA kuifuata NKANA FC Jumatano

Kikosi cha mabingwa wa Tanzania Bara Simba kinatarajiwa kuondoka Jumatano ijayo Disemba 12 kwenda nchini Zambia kwa ajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Nkana Fc.

Mchezo huo wa kwanza utapigwa Ijumaa ijayo, Disemba 14 Kitwe Zambia

Baada ya mchezo huo, Simba itarejea nchini tayari kwa mchezo wa marudiano utakaopigwa Disemba 21 katika dimba la Taifa.

Mabingwa hao wa nchi wameendelea kujifua kwenye uwanja wa Boko Veterans wakijiandaa na mchezo huo wa ugenini

Timu hiyo inayonolewa na kocha Patrick Aussems imedhamiria kutinga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu

Italikamilisha hilo kama itaibuka na ushindi wa jumla katika michezo hiyo miwili dhidi ya Nkana