Simba 1-2 Nkana FC : Full Time

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba wameanza kwa kupoteza mchezo wa awali wa michuano ya ligi ya mabingwa raundi ya kwanza baada ya kufungwa mabao 2-1 na Nkana FC.

Bao muhimu la ugenini la Simba lilifungwa kwa mkwaju wa penati na nahodha John Bocco kwenye dakika ya 73 baada ya Meddie Kagere kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari

Simba sasa inahitaji ushindi wa bao 1-0 nyumbani ili iweze kutinga hatua ya makundi.

Nkana Fc wamecheza vyema kwenye uwanja wao wa nyumbani na kufanikiwa kuibuka na ushindi huo.

Sasa ni zamu ya Simba nayo kuutumia vyema uwanja wa Taifa kwenye mchezo wa marudiano wiki ijayo.

Hakuna kisichowezekana, hii ni nafasi adimu kwa Simba kutinga hatua ya makundi ya michuano hii mikubwa kabisa barani Afrika katika ngazi ya vilabu