Timu ya Nkana Fc kutoka Zambia imewasili nchini usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa dhidi ya wenyeji wao Simba.
Mchezo huo utapigwa Jumapili Disemba 23, 2018 kwenye uwanja wa Taifa.
Nkana imekuja mapema kuliko ilivyotarajiwa viongozi wa timu hiyo wakidai wamefanya hivyo ili kupata muda wa kuzoea hali ya hewa ya joto katika jiji la Dar es salaam.
Wakati wapinzani wao wakiwasili, Simba leo inashuka katika dimba la Taifa kucheza na KMC kwenye mchezo wa kiporo wa ligi kuu ya Tanzania Bara.
Mchezo huo utapigwa saa 12 jioni