Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems leo anaweza kumtumia beki mpya wa kulia wa timu hiyo Zana Coulibaly kwenye mchezo dhidi ya KMC baada ya kibali chake kuwasili.
Coulibaly alitua Simba mwishoni mwa mwezi Novemba akitokea klabu ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast
Amekuwa akijifua katika kikosi cha Simba akisubiri kibali hicho cha uhamisho wa Kimataifa (ITC) ambapo uongozi wa Simba umethibitisha tayari kimewasili
“Zana Oumar Coulibaly anayo ruhusa kwa sasa kucheza Ligi kuu na kocha Patrick Aussems anayo nafasi ya kumpanga leo dhidi ya KMC ikimpendeza,” ilisema taarifa ya msemaji wa Simba, Haji Manara