
Wito huo umetolewa jana na Meneja wa Uwanja wa Taifa Nsajigwa Gordon ambaye amesema hatua hiyo inatokana na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kuagiza viwanja hivyo kufungwa ili kupisha marekebisho.
Viwanja hivyo vinatarajiwa kufungwa ili kupisha ukarabati tayari kwa michuano ya AFCON 19 ngazi ya vijana chini ya umri wa miaka 17 inayotarajiwa kuanza April 14-28 Tanzania ikiwa mwenyeji wa michuano hiyo
Sima imekuwa ikitumia uwanja wa Taifa kama uwanja wake wa nyumbani hivyo italazimika kutafuta uwanja mwingine kwa ajili ya michezo yake ya nyumbani kwa kipindi chote ambacho uwanja huo utakuwa umefungwa