Uwanja wa Taifa, Uhuru na Azam Complex kufungwa wakati wowote

Timu zinazotumia Uwanja wa Uhuru, Taifa na Azam Complex kwaajili ya michezo ya ligi mbalimbali zimeshauriwa kutafuta viwanja vingine kwa ajili ya michezo yao kutokana na viwanja hivyo kukaribia kufungwa kupisha ukarabati kuelekea kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Vijana.

Wito huo umetolewa jana na Meneja wa Uwanja wa Taifa Nsajigwa Gordon ambaye amesema hatua hiyo inatokana na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kuagiza viwanja hivyo kufungwa ili kupisha marekebisho.

Viwanja hivyo vinatarajiwa kufungwa ili kupisha ukarabati tayari kwa michuano ya AFCON 19 ngazi ya vijana chini ya umri wa miaka 17 inayotarajiwa kuanza April 14-28 Tanzania ikiwa mwenyeji wa michuano hiyo

Sima imekuwa ikitumia uwanja wa Taifa kama uwanja wake wa nyumbani hivyo italazimika kutafuta uwanja mwingine kwa ajili ya michezo yake ya nyumbani kwa kipindi chote ambacho uwanja huo utakuwa umefungwa