
Michezo 12 iliyosalia inaweza kuipa Yanga alama 36 na kuwafanya mabingwa hao wa kihistoria kuweza kufikisha alama 100
Habari njema kwa Yanga ni kuwa haina kibarua kikubwa sana cha michezo ya mikoani ukilinganisha na wapinzani wao katika mbio za ubingwa Simba
Simba iliyoshuka dimbani mara 20 bado ina deni la michezo 18 hivyo kuwafanya bado wawe na kazi kubwa licha ya kuwa na faida ya kimahesabu iwapo wataweza kushinda michezo yao yote
Yanga imebakiza michezo minne tu ya nje ya jiji la Dar es salaam huku michezo nane ikitarajiwa kupigwa uwanja wa Taifa
Michezo ya ugenini ambayo itapigwa nje ya jiji la Dar es salaam ni dhidi ya Mtibwa Sugar, Lipuli Fc, Ndanda na Biashara wakati michezo dhidi ya Azam Fc na Ruvu Shooting ni ya ugenini lakini itapigwa jijini Dar es salaam
Michezo iliyobaki ambayo Yanga ni mwenyeji ni dhidi ya KMC, African Lyon, Prisons, Mbeya City, Azam Fc na Kagera Sugar