
Kagere amewataka mashabiki kuiombea na kuiunga mkono timu kwa hali na mali ili kuhakikisha inatinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa
“Nawaambia wote wenye mapenzi mema na Simba, wale wanaoamini kuwa tunaweza kutinga robo fainali, nusu fainali na hata fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa, waungane nasi kwa kutuombea ili tuweze kufanikiwa,” amesema Kagera katika ujumbe mfupi alioutuma kwa mashabiki wa Simba
Simba inatarajiwa kwenda Algeria siku chache zijazo tayari kwa mchezo huo dhidi ya JS Saoura utakaopigwa Jumamosi, March 09